Timor ya Mashariki

Timor ya Mashariki (kwa Kireno Timor-Leste, kwa Kitetum Timór Lorosa'e; jina rasmiː República Democrática de Timor-Leste au Repúblika Demokrátika Timór-Leste) ni nchi ya Asia ya kusini-mashariki kwenye kisiwa cha Timor, takriban km 640 kaskazini kwa Darwin, Australia.

Timor ya Mashariki


Ramani

Eneo lake ni nusu ya mashariki ya kisiwa hicho pamoja na visiwa vya Atauro na Jaco. Kuna pia eneo dogo upande wa magharibi ya Timor ambao kwa kiasi kikubwa uko chini ya Indonesia pamoja na visiwa vya jirani.

Eneo lote la nchi ni km² 15,007.

Mji mkuu ni Dili wenye wakazi 245,000.

Timor ya Mashariki ni kati ya nchi maskini zaidi duniani.

Historiahariri

Wakazi ni mchanganyiko wa Wapapua-Wamelanesia waliofika miaka 40,000 iliyopita, Waaustronesia waliofika kama mwaka 3000 KK na Wamalay waliokuwa wa mwisho.

Timor ilikuwa kituo cha biashara cha Wareno tangu karne ya 16. Maeneo mengine ya visiwa vya Indonesia ya leo yalivamiwa na Waholanzi na Timor ilibaki kisiwa pekee chini ya utawala wa Ureno katika sehemu hii ya dunia.

Katika karne ya 19 Waholanzi walifika pia Timor. Mikataba ya 1859 na 1916 zilithibitihsa ugawaji wa kisiwa. Sehemu ya magharibi ilikuwa chini ya Uholanzi na baadaye sehemu ya Indonesia, lakini sehemu ya mashariki ilibaki koloni la Ureno.

Baada ya mapinduzi ya Ureno ya 1974 Wareno waliondoka Timor bila maandalizi na kutosha. Viongozi wazalendo walitangaza uhuru. Lakini siku chache baada ya tangazo hilo, jeshi la Indonesia lilivamia nchi ambayo ikatangazwa kuwa jimbo la Indonesia. Hali hii haikutambuliwa na Umoja wa Mataifa.

Vita vikali vya msituni vilifuata kati ya wapigania uhuru na jeshi la Indonesia.

Mabadiliko yalipatikana mwaka 1998 baada ya rais Suharto wa Indonesia kujiuzulu, na rais mpya Bacharuddin Jusuf Habibie kuwa tayari kuipa Timor ya Mashariki hali ya kujitawala ndani ya Indonesia.

Karibu wananchi wote (98 %) walihudhuria katika kura ya maoni ya tarehe 30 Agosti 1999 na zaidi ya robo tatu (78,5 %) walipigia kura uhuru badala ya kuwa jimbo la kujitawala.

Baada ya kura hii jeshi la Indonesia lililipiza kisasi kwa kuua watu wengi na kuharibu nyumba lakini macho ya dunia yalitazama Timor, na serikali ya Indonesia kwa tishio la kufutiwa mikopo ya benki ya dunia ililazimishwa kuondoa jeshi lake na kukubali kufika kwa jeshi la Umoja wa Mataifa chini ya uongozi wa Australia.

Tangu tarehe 27 Septemba 2002 Timor ya Mashariki ni nchi mwanachama wa UM.

Watuhariri

Kuna lugha 19 ambazo huzungumzwa nchini Timor ya Mashariki.Lugha rasmi ni Kitetum (lugha mama ya 30.6% za wakazi), ambacho ni kati ya lugha za Austronesia, pamoja na Kireno.

Upande wa dini, wananchi karibu wote (99.53%) ni wafuasi wa Yesu Kristo katika Kanisa Katoliki (97.57%) na madhehebu ya Uprotestanti (1.96%). Wengi walijiunga na Kanisa wakati wa vita vya ukombozi. Waislamu ni 0.24%.

Tazama piahariri

Viungo vya njehariri

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Taarifa za jumla
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Timor ya Mashariki kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoPasakaPasaka ya KikristoAlhamisi kuuAngkor WatOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoFasihi simuliziUbuntuOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaNgeli za nominoTanzaniaFasihiShairiIjumaa KuuMikoa ya TanzaniaLughaHomanyongo CJumuiya ya Afrika MasharikiKamusi za KiswahiliMofimuAina za manenoVivumishiModule:ArgumentsUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaSilabiNembo ya TanzaniaKiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaDiamond PlatnumzOrodha ya makabila ya TanzaniaMaumivu ya kiunoOrodha ya Watakatifu WakristoKitenziDuniaKumaVitendawiliTamthiliaIndonesiaTafsiriNominoTendo la ndoaSentensiUandishi wa ripotiTanganyikaUwanja wa Taifa (Tanzania)Orodha ya nchi za AfrikaNguzo tano za UislamuHistoria ya KanisaNomino za pekeeYouTubeMuhammadHistoria ya KiswahiliJohn MagufuliVieleziBaike: Msaada wa kuanzisha makalaAmri KumiMaalum:MabadalikoyaKaribuniMbooWasukumaMshororoMawasilianoKisaweHafidh AmeirFasihi andishiTarakilishiDizasta VinaLigi ya Mabingwa AfrikaBendera ya TanzaniaSiku tatu kuu za PasakaSimba S.C.Young Africans S.C.UkimwiOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaOrodha ya Marais wa TanzaniaOrodha ya Magavana wa TanganyikaKiraiBaike: AboutOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaTashdidiKitenzi kishirikishiStadi za lughaAsili ya KiswahiliJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaRamaniHistoria ya AfrikaAfrika ya Mashariki ya KijerumaniWilaya za TanzaniaMisimu (lugha)WachaggaMfumo wa JuaAgano la KaleKamusi ya Kiswahili sanifuMziziKwaresimaNomino za dhahaniaKamusiTabianchiAlama ya uakifishaji