Mikoa ya Senegal

(Elekezwa kutoka Regions of Senegal)

Mikoa ya Senegal ni ngazi ya kwanza ya ugatuzi nchini Senegal katika Afrika ya Magharibi. Senegal imegawanywa katika mikoa 14 (kwa Kifaransa: régions). Kila mkoa unasimamiwa na halmashauri yake (Conseil Régional) ambayo wajumbe wake wanachaguliwa na wananchi kwenye ngazi ya tarafa.

Mikoa ya Senegal

Ngazi ya pili ya ugatuzi ni wilaya (departements) 45, tarafa (arrondissements) 103 (ambazo hazina kazi ya kiutawala) na maeneo ya jumuiya za kieneo (collectivités locales) ambazo huchagua maafisa wa utawala.

Orodha ifuatayo inaonyesha mikoa ya Senegal pamoja na idadi ya wakazi kufuatana na sensa ya mwaka 2013.[1]

MkoaMakao makuuEneo
(km²)
Wakazi
(sensa 2013)
DakarDakar5473,137,196
ZiguinchorZiguinchor7,352549,151
DiourbelDiourbel4,8241,497,455
Saint-LouisSaint-Louis19,241908,942
TambacoundaTambacounda42,364681,310
KaolackKaolack  5,357960,875
ThièsThiès6,6701,788,864
LougaLouga24,889874,193
FatickFatick6,849835,352
KoldaKolda13,771714,392
MatamMatam29,445562,539
KaffrineKaffrine11,262566,992
KédougouKédougou16,800152,357
SédhiouSédhiou7,341452,944
Jengo la Halmashauri ya Mkoa huko Ziguinchor. Mikoa huwa na madaraka ya kikatiba nchini Senegal, tofauti na wilaya na tarafa.

Marejeohariri

  1. Senegal: Administrative Division, tovuti ya Citypopulation.de, iliangaliwa Januari 2022
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoPasakaPasaka ya KikristoAlhamisi kuuAngkor WatOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoFasihi simuliziUbuntuOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaNgeli za nominoTanzaniaFasihiShairiIjumaa KuuMikoa ya TanzaniaLughaHomanyongo CJumuiya ya Afrika MasharikiKamusi za KiswahiliMofimuAina za manenoVivumishiModule:ArgumentsUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaSilabiNembo ya TanzaniaKiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaDiamond PlatnumzOrodha ya makabila ya TanzaniaMaumivu ya kiunoOrodha ya Watakatifu WakristoKitenziDuniaKumaVitendawiliTamthiliaIndonesiaTafsiriNominoTendo la ndoaSentensiUandishi wa ripotiTanganyikaUwanja wa Taifa (Tanzania)Orodha ya nchi za AfrikaNguzo tano za UislamuHistoria ya KanisaNomino za pekeeYouTubeMuhammadHistoria ya KiswahiliJohn MagufuliVieleziBaike: Msaada wa kuanzisha makalaAmri KumiMaalum:MabadalikoyaKaribuniMbooWasukumaMshororoMawasilianoKisaweHafidh AmeirFasihi andishiTarakilishiDizasta VinaLigi ya Mabingwa AfrikaBendera ya TanzaniaSiku tatu kuu za PasakaSimba S.C.Young Africans S.C.UkimwiOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaOrodha ya Marais wa TanzaniaOrodha ya Magavana wa TanganyikaKiraiBaike: AboutOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaTashdidiKitenzi kishirikishiStadi za lughaAsili ya KiswahiliJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaRamaniHistoria ya AfrikaAfrika ya Mashariki ya KijerumaniWilaya za TanzaniaMisimu (lugha)WachaggaMfumo wa JuaAgano la KaleKamusi ya Kiswahili sanifuMziziKwaresimaNomino za dhahaniaKamusiTabianchiAlama ya uakifishaji