Rais

Rais (kutoka Kiarabu: رئیس) ni cheo cha mkuu wa nchi katika serikali ya jamhuri, na pengine mkuu wa taasisi fulani ("mwenyekiti").

Rais wa Tanzania, John Magufuli (Kulia) akiwa na Dr. Salem Al Ismaily wa Oman

Rais wa nchi huwa anachaguliwa ama na wananchi wote au na bunge. Katika nchi kadhaa kuna pia mkutano maalumu unaoitishwa kwa uchaguzi wa rais pekee, kama vile Marekani[1] au Ujerumani [2].

Kuna aina mbili za rais kufuatana na katiba za nchi mbalimbali:

Katika muundo wa serikali ya kibunge shughuli za serikali zinasimamiwa na waziri mkuu. Madaraka ya rais katika muundo huo hufanana na madaraka ya mfalme wa kikatiba isipokuwa hayupo kama rais kwa muda wa maisha yake kama mfalme.

Katika nchi chache, yaani Uswisi, San Marino na Uruguay, kazi za rais hazitekelezwi na mtu mmoja bali na kamati ya viongozi kwa ujumla, kama Halmashauri ya Shirikisho ya Uswisi.

Marejeo

  1. Katika Marekani wananchi wanapigia kura wajumbe wa "electoral college" na hao wanamchagua rais wakikutana mara moja tu
  2. Ujerumani mkutano maalumu wa "Bundesversammlung" unafanywa na wabunge wote wa Bundestag na idadi sawa ya wawakilishi wa mabunge ya majimbo wanaokutana pamoja kwa uchaguzi wa rais pekee.
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoPasakaPasaka ya KikristoAlhamisi kuuAngkor WatOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoFasihi simuliziUbuntuOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaNgeli za nominoTanzaniaFasihiShairiIjumaa KuuMikoa ya TanzaniaLughaHomanyongo CJumuiya ya Afrika MasharikiKamusi za KiswahiliMofimuAina za manenoVivumishiModule:ArgumentsUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaSilabiNembo ya TanzaniaKiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaDiamond PlatnumzOrodha ya makabila ya TanzaniaMaumivu ya kiunoOrodha ya Watakatifu WakristoKitenziDuniaKumaVitendawiliTamthiliaIndonesiaTafsiriNominoTendo la ndoaSentensiUandishi wa ripotiTanganyikaUwanja wa Taifa (Tanzania)Orodha ya nchi za AfrikaNguzo tano za UislamuHistoria ya KanisaNomino za pekeeYouTubeMuhammadHistoria ya KiswahiliJohn MagufuliVieleziBaike: Msaada wa kuanzisha makalaAmri KumiMaalum:MabadalikoyaKaribuniMbooWasukumaMshororoMawasilianoKisaweHafidh AmeirFasihi andishiTarakilishiDizasta VinaLigi ya Mabingwa AfrikaBendera ya TanzaniaSiku tatu kuu za PasakaSimba S.C.Young Africans S.C.UkimwiOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaOrodha ya Marais wa TanzaniaOrodha ya Magavana wa TanganyikaKiraiBaike: AboutOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaTashdidiKitenzi kishirikishiStadi za lughaAsili ya KiswahiliJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaRamaniHistoria ya AfrikaAfrika ya Mashariki ya KijerumaniWilaya za TanzaniaMisimu (lugha)WachaggaMfumo wa JuaAgano la KaleKamusi ya Kiswahili sanifuMziziKwaresimaNomino za dhahaniaKamusiTabianchiAlama ya uakifishaji