Maambukizo

Maambukizo humaanisha kuingia kwa vidubini katika mwili geni kama vidubini hivi vinabaki, vinazaa na kuenea.

Maambukizo mara nyingi yanasababisha magonjwa yanayoitwa "magonjwa ya kuambukiza".

Vidubini vya faida na vya hasarahariri

Si lazima kila ambukizo lisababishe ugonjwa, lakini magonjwa mengi ni magonjwa ya kuambukiza.

Kuna vidubini ambavyo vinaishi ndani ya mwili wa binadamu bila kusababisha hasara; kuna hata vidubini ambavyo ni muhimu kwa maisha na afya ya binadamu, kwa mfano bakteria nyingi zinazoishi ndani ya utumbo na kusaidia Mmeng'enyo wa chakula.

Lakini vingine vinaweza kusababisha hasara ama kwa sababu vinatoa sumu fulani au kwa sababu vinasababisha upinzani mkali wa mfumo wa kinga wa mwili ambao ni hatari kama idadi ya vidubini vyenye hasara ni kubwa sana au vikiongezeka haraka mno. Vidubini hivi vyenye uwezo wa kuleta hasara huitwa "pathojeni" (kutoka Kiingereza pathogen) yaani "sababishi mateso".

Ambukizohariri

Ambukizo hutokea kama vidubini hatari vinaingia mwilini, kukuta mazingira vinapoweza kustawi na kuongezeka. Uvamizi wa vidubini vya nje kwenye mwili hutokea kila siku mara nyingi maana hewa tunaopumua, vitu tunavyogusa na chakula tunachokula, vyote vimejaa uhai kwa umbo la bakteria, virusi na kadhalika.

Mara nyingi mfumo wa kinga mwilini unatambua vidubini vya kigeni na kuviharibu bila sisi wenyewe kutambua hali isiyo kawaida. Lakini hata kama kinga wa mwili ni dhaifu, kama vidonda vya ngozi au utando telezi vinaruhusu kufika kwa vidubini mahali pasipo mfumo wa kinga imara, viini hivi vinaweza kusambaa na kuongezeka.

Hapo maitikio ya mfumo wa kinga yanaongezeka mara nyingi hadi kushinda wavamizi. Lakini itikio hili linakuja mara nyingi pamoja na dalili kali tunayoona kama dalili za ugonjwa k.mf. homa, maumivu na udhaifu. Katika hali hii ya kupambana na vidubini fulani mwili wote unaweza kudhoofika zaidi na kushambuliwa tena na viini vingine.

Hapo mashambulio yanaweza kushinda kinga ya mwilini na kusababisha hasara za kudumu hadi kifo. Siku hizi kuna madawa mbalimbali yanayosaidia mapambano dhidi ya vidubini hatari na hivyo kuwezesha mfumo wa kinga mwilini kumaliza wavamizi.

Njia za maambukizo zinatofautiana. Mafua husababishwa na virusi zinazoweza kutoka mwilini mwa mgonjwa anayekohoa au virusi zinaweza kuvuka umbali mdogo kwa hiyo watu wa karibu wanaweza kupokea vidubini hivi bila kumgusa mtu.

Maambukizo yanaweza kutokea kwa njia ya bakteria fulani zinazoweza kudumu nje ya mwili kwa mudu fulani; ilhali hazionekani inatosha kama mtu anagusa mahali penye bakteria hizi na baadaye kuingiza kidole mdomoni.

Virusi za UKIMWI ni za hatari kwa sababu ya ugumu wa tiba lakini ni dhaifu; haziwezi kudumu hata kidogo nje ya mwili, kwa hiyo zinamhitaji mtu mwenye Ukimwi kuwa karibu sana na mtu mwingine ili viowevu vya mwili kama damu au shahawa viweze kupita kutoka mmoja hadi mwingine bila kupoa.

Aina za vidubini hatarihariri

Vidubini vinavyoweza kuingia katika mwili geni, kuenea mle na kusababisha hasara ni hasa

Mifano ya magonjwa ya kuambukiza yanayosababishwa na vidubini hatarihariri

Magonjwa ya kuambukiza yaliyosababishwa na bakteriahariri

Magonjwa ya kuambukiza yaliyosababishwa na virusihariri

Magonjwa ya kuambukiza yaliyosababishwa na fungihariri

  • nyungunyungu ya ngozi (athlete's foot)

Magonjwa ya kuambukiza yaliyosababishwa na vimeleahariri

Maambukizo katika kompyutahariri

Lugha ya maambukizo imeanza kutumiwa pia nje ya biolojia kwa ajili ya vurugu katika kompyuta inayosababishwa kwa kuingia kwa programu ya kigeni zinazoitwa "virusi ya kompyuta".

Viungo vya njehariri

🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoPasakaPasaka ya KikristoAlhamisi kuuAngkor WatOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoFasihi simuliziUbuntuOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaNgeli za nominoTanzaniaFasihiShairiIjumaa KuuMikoa ya TanzaniaLughaHomanyongo CJumuiya ya Afrika MasharikiKamusi za KiswahiliMofimuAina za manenoVivumishiModule:ArgumentsUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaSilabiNembo ya TanzaniaKiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaDiamond PlatnumzOrodha ya makabila ya TanzaniaMaumivu ya kiunoOrodha ya Watakatifu WakristoKitenziDuniaKumaVitendawiliTamthiliaIndonesiaTafsiriNominoTendo la ndoaSentensiUandishi wa ripotiTanganyikaUwanja wa Taifa (Tanzania)Orodha ya nchi za AfrikaNguzo tano za UislamuHistoria ya KanisaNomino za pekeeYouTubeMuhammadHistoria ya KiswahiliJohn MagufuliVieleziBaike: Msaada wa kuanzisha makalaAmri KumiMaalum:MabadalikoyaKaribuniMbooWasukumaMshororoMawasilianoKisaweHafidh AmeirFasihi andishiTarakilishiDizasta VinaLigi ya Mabingwa AfrikaBendera ya TanzaniaSiku tatu kuu za PasakaSimba S.C.Young Africans S.C.UkimwiOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaOrodha ya Marais wa TanzaniaOrodha ya Magavana wa TanganyikaKiraiBaike: AboutOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaTashdidiKitenzi kishirikishiStadi za lughaAsili ya KiswahiliJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaRamaniHistoria ya AfrikaAfrika ya Mashariki ya KijerumaniWilaya za TanzaniaMisimu (lugha)WachaggaMfumo wa JuaAgano la KaleKamusi ya Kiswahili sanifuMziziKwaresimaNomino za dhahaniaKamusiTabianchiAlama ya uakifishaji