Guyani ya Kifaransa

Département ya Ufaransa

(Elekezwa kutoka Guyana ya Kifaransa)
Guyane
Lagwiyann
Nembo
Jina la KifaransaGuyane
(kwa Krioli:Lagwiyann)
Jina la kawaidaGuyani ya Kifaransa
Mji MkuuKayeni
Eneo86 504 km²
Mkuu wa MkoaGabriel Serville
Idadi ya wakazi301 099
Sensa ya mwaka2022
Wakazi kwa km²3.2
Wilaya (arrondissements)3
Ramani
-- Kwa nchi jirani angalia makala Guyana--

Guyani ya Kifaransa (kwa Kifaransa: Guyane française au Guyane tu, kwa Krioli ya Guyani ya Kifaransa Lagwiyann) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa ("département d'outre-mer" au DOM) katika Amerika Kusini. Makao makuu ya Guyana ni mji wa Kayeni.

Imepakana na Brazil na Surinam. Pwani ya Bahari ya Karibi (Atlantiki) iko upande wa kaskazini.

Eneo la Guyani ni mojawapo ya mikoa tisa ya nje zaidi (OR) ya Umoja wa Ulaya. Ni eneo pekee la bara la Ufaransa na Umoja wa Ulaya huko Amerika Kusini na eneo la mwisho la Ufaransa katika bara la Amerika.

Ilikuwa koloni la Ufaransa; sasa imekuwa sehemu kamili ya Ufaransa kisiasa na kisheria. Wakazi ni raia wa Ufaransa. Eneo lina hali ya mkoa (fr:département) na pia kanda (fr:région) katika Ufaransa. Hivyo Guyani ni sehemu ya Umoja wa Ulaya. Pesa yake ni Euro.

Watu

Idadi ya wakazi imekadiriwa kuwa 296,711 katika mwaka 2019 na inaendelea kuongezeka kwa uzazi na uhamiaji.

Wakazi walio wengi ni wa asili ya Afrika au machotara wa mchanganyiko wa Kiafrika-Kizungu (Wakrioli) (60-70%). Asilimia 14 ni Wazungu, hasa kutoka Ufaransa; wengine ni Waindio asilia (3-4%), Wachina (3-4%), Wahindi na wahamiaji wa hivi karibuni kutoka Laos (1-2%), Vietnam, Lebanoni n.k.

Lugha rasmi na ya kawaida ni Kifaransa.

Upande wa dini, wakazi walio wengi ni Wakristo wa Kanisa Katoliki (66.7%).

Tazama pia

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyani ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guyani ya Kifaransa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoPasakaPasaka ya KikristoAlhamisi kuuAngkor WatOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoFasihi simuliziUbuntuOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaNgeli za nominoTanzaniaFasihiShairiIjumaa KuuMikoa ya TanzaniaLughaHomanyongo CJumuiya ya Afrika MasharikiKamusi za KiswahiliMofimuAina za manenoVivumishiModule:ArgumentsUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaSilabiNembo ya TanzaniaKiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaDiamond PlatnumzOrodha ya makabila ya TanzaniaMaumivu ya kiunoOrodha ya Watakatifu WakristoKitenziDuniaKumaVitendawiliTamthiliaIndonesiaTafsiriNominoTendo la ndoaSentensiUandishi wa ripotiTanganyikaUwanja wa Taifa (Tanzania)Orodha ya nchi za AfrikaNguzo tano za UislamuHistoria ya KanisaNomino za pekeeYouTubeMuhammadHistoria ya KiswahiliJohn MagufuliVieleziBaike: Msaada wa kuanzisha makalaAmri KumiMaalum:MabadalikoyaKaribuniMbooWasukumaMshororoMawasilianoKisaweHafidh AmeirFasihi andishiTarakilishiDizasta VinaLigi ya Mabingwa AfrikaBendera ya TanzaniaSiku tatu kuu za PasakaSimba S.C.Young Africans S.C.UkimwiOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaOrodha ya Marais wa TanzaniaOrodha ya Magavana wa TanganyikaKiraiBaike: AboutOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaTashdidiKitenzi kishirikishiStadi za lughaAsili ya KiswahiliJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaRamaniHistoria ya AfrikaAfrika ya Mashariki ya KijerumaniWilaya za TanzaniaMisimu (lugha)WachaggaMfumo wa JuaAgano la KaleKamusi ya Kiswahili sanifuMziziKwaresimaNomino za dhahaniaKamusiTabianchiAlama ya uakifishaji